2013-02-26 14:56:23

Sadaka ya Ijumaa kuu ijenge na kuimarisha mshikamano wa kiimani na Wakristo wanaoishi katika Nchi Takatifu


Baraza la Kipapa la Makanisa ya Mashariki limewaandikia Barua Mabalozi wa Vatican sehemu mbali mbali za dunia kuhimiza mchango wa waamini unaotolewa wakati wa Ijumaa kuu, kama kielelezo cha mshikamano wa dhati na waamini wanaoishi katika Nchi Takatifu.
Hawa ni wale ambao wamebaki na wanaendelea kutunza maeneo matakatifu, kwani walibahatika kupata urithi wa imani. Katika Maadhimisho ya Mwaka wa Imani, tukio hili la mshikamano lipewe msukumo wa pekee na Makanisa mahalia.
Kipindi cha Kwaresima, kiwe ni sehemu ya maandalizi kwa ajili ya kuchangia kwa ukarimu na upendo kwa wale wanaoishi katika Nchi Takatifu, kwa hali na mali. Waamini wahamasishwe kushiriki katika tendo hili ambalo limekuwa likipewa msukumo wa pekee na Viongozi wa Kanisa. Ni mchango unaopania anasema Kardinali Leonardo Sandri kusaidia mchakato wa maendeleo endelevu katika Nchi Takatifu na kwenye Makanisa yaliyoko Mashariki.








All the contents on this site are copyrighted ©.