2013-02-23 14:07:33

Rais Giorgio Napolitano aagana na Papa Benedikto XVI mjini Vatican


Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, Jumamosi tarehe 23 Februari 2013 baada ya kutoka kwenye Mafungo ya kiroho, amekutana na kuzungumza na Rais Giorgio Napolitano pamoja na ujumbe wake mjini Vatican. Mazungumzo ya viongozi hawa wawili yalikuwa ni mazito na yenye kuonesha urafiki wa dhati baina ya viongozi hawa ambao wamefahamiana na kushirikiana kwa muda mrefu.

Rais Napolitano amemshukuru Baba Mtakatifu kwa niaba ya wananchi wa Italia kwa uwepo wake wa karibu katika nyakati mbali mbali. Wanatambua na kuthamini mchango na mafundisho ya Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita katika masuala ya kidini na kimaadili, wanaahidi kwamba, wataendelea kumsindikiza katika maisha yake kwa njia ya sala.

Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, kwa upande wake, amemshukuru sana Rais Giorgio Napolitano pamoja na mkewe kwa urafiki wao na kuitakia Italia ufanisi mkubwa kwa ajili ya mafao ya wengi, hasa wakati huu Italia inapofanya uchaguzi mkuu wa viongozi wake, dhamana fungamanishi.







All the contents on this site are copyrighted ©.