2013-02-23 08:18:55

Jopo la Marais wastaafu kushughulikia mgogoro wa mpaka kati ya Tanzania na Malawi


Waziri wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa nchini Malawi Bwana Patrick Kabambe amesema kwamba, mgogoro wa mpaka kati ya Tanzania na Malawi unatarajiwa kusuluhishwa na viongozi wakuu watatu kutoka Afrika. Viongozi hao ni: Rais mstaafu Joachim Chisano wa Msumbiji, Rais mstaafu Thabo Mbeki wa Afrika ya Kusini na Rais mstaafu Festus Mogae wa Botswana.

Viongozi wa Malawi na Tanzania tayari wamekwisha wasilisha hoja na misimamo ya nchi zao kuhusu mgogoro wa mpaka kati ya Tanzania na Malawi. Jopo la Marais wastaafu kutoka Afrika linatarajia kuanza kutekeleza kazi yake mwishoni mwa mwezi Februari, 2013. Mgogoro huu ulishika kasi na kuingia katika medani za kimataifa pale Malawi ilipotoa idhini kwa kampuni moja ya kimataifa kuanza kuchimba mafuta kwenye Ziwa Nyasa kwa madai kwamba, Ziwa lote ni mali yao.







All the contents on this site are copyrighted ©.