2013-02-21 15:26:41

Tamko kuhusu mabadiliko katika Conclave-- Pd. Lombardi


Katika mkutano wa wanahabari wa mapema siku ya Jumatano, Mkurugenzi wa Ofisi ya Uchapishaji ya Vatican na msemaji wa Papa , Padre Federico Lombardi, alieleza kwamba, Papa Benedikto XV1, anafikiri kuchapisha tamko lake binafsi(Motu Prioprio) hivi karibuni , kwa nia ya kutoa ufafanuzi katika vipengere kadhaa vya sheria zinazo tawala wakati Kiti cha Petro kitakapo kuwa wazi na pia juu kikao cha Makardinali cha kuchagua Papa Mpya (Conclave).
Na kwamba ufafanuzi huo, kama ataufanya itakuwa kabla ya kujiuzuru kwake rasmi hapo tarehe 28 Februari.

Padre Federico Lombardi anafikiri hati hiyo ya Papa Benedikto,pengine itatoa ufafanuzi juu ya vipegere kadhaa kwa ajili ya kuainisha sheria kadhaa zinazotumika wakati Kiti cha Petro kinapokuwa wazi na pia Conclave. Na kwamba , uainishaji huo unategemea maamuzi yake Papa, vinginevyo kwa wakati huu sheria zote zinabaki kama zilivyo.

Hivyo mpaka sasa, Kardinali Tarcisio Bertone, Katibu wa Vatican, aliyeteuliwa kuwa Camerlengo hapo April 4, 2007, ndiye atakuwa Msimamizi mkuu wa jimbo la Papa na Kanisa la Ulimwengu, wakati wote Kiti cha Petro kitakapobaki wazi, baada ya Papa Benedikto XV1, kujiuzuru rasmi, saa mbili za usiku, tarehe 28 Februari, 2013, hadi hapo Khalifa mwingine atakapochaguliwa.
Pia kwa cheo hicho, Kardinali Tarcisio anakuwa ni kiongozi Mkuu wa Mahakama ya Kitume na sahihi ya Kitume, pia Mtunzaji na msimamizi mkuu wa mali na haki za Jimbo Takatifu katika muda huo wa utupu.
Katika kipindi hiki, kwa mujibu wa sheria ya "Universi Dominici Gregis", wanaohusika na utendaji wa kazi za jimbo la Papa katika ngazi mbalimbali hata walioteuliwa na Papa, hawapotezi nafasi zao , bali wanaendelea na majukumu yao kama kawaida, chini ya Decania ya Makardinali, kama walivyokuwa wakiwajibika kwa Baba Mtakatifu Mwenyewe.

Katiba hiyo inaeleza, mihuri na yaliyomo katika chumba Papa,licha ya chumba cha Papa kufungwa rasmi, wafanyakazi wa kawaida wanaohudumia katika makao binafsi ya Papa, wanaweza kukaa mpaka hadi hapo baada ya mazishi, au kuteuliwa kwa Papa Mpya.

Usimamizi wote kazi na uwajibikaji, katika kipindi cha Kiti cha Petro kuwa wazi, unaogozwa na Camerlengo akisaidiana na Makardinali wengine watatu, hasa katika utatauzi wa masuala madogomadogo lakini muhimu , kama ilivyoelezwa katika sheria za kanisa ( Ibara ya 7).

Jopo hilo la Camerlengo na wasaidizi wake Makardinali watatu, wanayo mamlaka ya kuamua lini waanze Mkutano wa dekania ya Makardinali kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi wa Papa, kwa mujibu wa Ibara namba 11.

Ni wajibu wa Camerlengo na pamoja na wasaidizi wake watatu Makardinali kusimamia utendaji wote wa wakati huo na kutunza siri zote za wakati wa upigaji kura katika mkutano wa conclave, unaofanyika katika kikanisa cha Sistine,cha ndani ya jengo la Kipapa la Vatican. Na pia camerlengo ndiye anahusika na hatua ya kuchoma makaa yenye kutoa moshi mweupe na kumtagaza Papa mpya alyechaguliwa na Makardinali katika kikao hicho cha Conclave.







All the contents on this site are copyrighted ©.