Papa kukutana na Makardinali watakaokuwepo Roma, 28 Februari 2013
Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, hapo tarehe 28 Februari 2013, kuanzia saa
5:00 asubuhi, atafanya mazungumzo ya faragha na kila Kardinali atakayekuwepo mjini
Roma kwa wakati huo na baadaye atakutana na Makardinali wote kwa pamoja.
Hii
itakuwa ni mara ya mwisho kwa Dekania ya Makardinali kuweza kuzungumza ana kwa ana
na Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita kama Khalifa wa Mtakatifu Petro.