2013-02-20 15:15:49

Historia ya maisha ni nafasi ya kukutana na Mungu


Kardinali Gianfranco Ravasi, Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Utamaduni, katika siku ya tatu ya tafakari na mafungo ya Kiroho kwa Wakazi wa jengo la Kipapa na wafanyakazi wa Curia ya Roma, alitazama zaidi matukio ya kanisa ya kihistoria na maelezo ya juu ya Masiya katika Zaburi.
Kardinali Ravasi , ameitaja historia kuwa ni mahali pa kukutana na Mungu. Historia inatuonyesha jinsi tunavyoweza kukutana na Mungu kupitia matukio mbalimbali kwenye hali zote , uchungu na mateso katika maisha na furaha pia, kama ilivyojionyesha katika historia ya mwana wa Mungu, aliyemwilishwa na kuja kukaa kwetu.
Katika kuyatafakari maisha ya mtu, historia yake daima, inakuwua ni nafasi inayo faa kukutana na Bwana Mungu wetu. Inaweza ikawa kupitia kashfa au madhulumu, hata katika nchi ambamo kwa mara nyingi tunauona ukimya wa Mungu, na pia katika mataifa ambako ukana Mungu umeshamiri.
Aliendelea kufafanua kwamba, hata katika kiini cha mema yote, tunapaswa kupata utambuzi kwamba , historia si tu mfulululizo wa matukio yasiyokuwa na maana,hata katika utendaji wetu mdogomdogo, na pengine katika majaribu na masumbufu, kama tunavyosoma katika kitabu cha Ayabu, yote hufanyika kwa mapenzi ya Mungu. Na kwa namna hiyo, binadamu huweza kuiimarisha imani yake na kusadiki zaidi kwamba, yupo mwenye uweza zaidi, anayetusindikiza katika hija yetu hapa duniani. Ni Yeye Mchungaji anayetulinda dhidi ya kila asili na historia za hatari, anayeandamana nasi katika safari ya kuelekea katika uhuru kamili.
Na kwamba, tunapaswa kuishi kwa tumaini, tumaini lisiolobadilika . Mungu wetu kama ilivyoelezwa katika Kitabu cha Kutoka sura ya tatu , Ni mungu asiyekuwa na Jina , ni Mimi niko na ambaye niko, kama alivyomwambia Musa, ndivyo utakavyo waambia wana wa Israel , "Mimi niko", ndiye aliyenituma. Na hivyo kumbe , binadamu anayeiishi na kulikubali neno hili anajenga mahusiano yake na Yeye aliyeko , katika uaminifu wake na katika mazungumzano nae na katika kukutana na kuishi pamoja.








All the contents on this site are copyrighted ©.