2013-02-19 15:28:42

SECAM -yatoa barua ya kichungaji juu ya Utawala kwa viongozi wa Afrika.


Maaskofu Katoliki wanachama wa SECAM, chombo kinachounganisha Mabaraza ya Mabaraza la Maaskofu Barani Afrika na Madagascar, wametoa barua yao ya kichungaji kwa viongozi wa Afrika, juu ya utawala bora, na kwa ajili ya ufanikishaji mazuri kwa wote katika kipindi cha mpito kuelekea demokrasia Afrika.

Barua hiyo ni wito kwa viongozi wa kisiasa , kutenda kwa haki kwa ajili ya kuijenga jamii ya Afrika iliyo bora zaidi na siyo tu kwa manufaa ya wasomi bali raia wote. Maaskofu wametoa barua hiyo ya kurasa 16, kama matokeo ya kukamilika kwa Mkutano wao wa hivi karibuni mjini Accra. Barua iliyotiwa sahihi na Rais wa SECAM, Kardinali Plycarp Pengo , Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam.

Maaskofu wanawasisitiza viongozi wa Afrika kukataa utendaji wowote ule, unaolenga kuvuruga matokeo halali ya chaguzi kuu na kila aina ya uozo na ufisadi, badala yake, waweke kipaumbele cha kwanza, mipango ya kufuta ufukara. Aidha viongozi wa Afrika ni lazima wahakikishe uwepo wa utaratibu katika miliki na mgao mzuri wa maliasili ya Bara la la Afrika, ili maliasili iwe ni kwa manufaa watu wote.

Askofu Mkuu Gabriel Mbilingi wa Jimbo Kuu la Lubango Angola, ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Secam, akirejea barua hiyo, juu ya utawala: kwa ajili ya mazuri kwa wote na demokrasia barani Afrika , ameeleza kwa kifupi yaliyomo kwamba, ni utetezi wa mazuri na heshima kwa haki za binadamu na ukuzaji wa utawala bora kama kipingere muhimu cha Kiinjili.
Na kwamba Kanisa ni wajibu wake kusimiamia amani katika mapito ya kisasa barani Afrika, kwa ajili ya uaptikanaji wa uhuru , maridhiano na ukarabati wa kweli. Kanisa pia linaunga mkono maamuzi yanayolenga kuheshimu utu wa binadamu na ushiriki wake katika maamuzi yanayoleta usawa na mwelekeo mzuri wa ustawi wa maisha ya wana wa Afrika.
Na kwamba, barua hii, ni uvuvio kutoka hati ya Kipapa ya "Africae Munis", iliyotolewa kama matokeo ya Sinodi ya Maaskofu ya Pili kwa Afrika, vipengere namba 23 hadi 29 vya hati hiyo, ambamo kwa kifupi mnaelezwa kwamba amani si tu zawadi ya kupokea lakini ni uwajibikaji katika utendaji wa kujenga amani ya kweli, kama sharti la lazima, kuwa na ufahamu wakutosha katika uvumilivu, huruma, mshikamano na udugu ndani ya jumuiya na jamii kwa ujumla.
Ni muhimu kujali kuinua utambuzi katika ngazi za kitaifa na kimataifa, na kutafuta mfumo unaofaa kwa ajili ya mgao wa utajiri wa maliasili na ukuzaji wa ushirikiano kwa ajili ya maendeleo na katika kupata majawabu yanayofaa wakati kunapotokea kutokuelewana.
Utume wa SECAM, hulenga kulikuza Kanisa kama familia ya Mungu barani Afrika , kudumisha na kukuza mawasiliano , ushirikiano na kutenda kwa pamoja kama Baraza la Maaskofu Katoliki Afrika . Na pia kuendeleza ushirikiano na serikali na taasisi zingine katika mwingiliano wa Maendeleo ya watu wa Afrika.








All the contents on this site are copyrighted ©.