2013-02-16 07:52:55

Wakili Ernst Von Freyberg ateuliwa kuwa Rais wa Benki ya Vatican


Tume ya Makardinali inayosimamia na kuongoza Benki ya shughuli za kidini mjini Vatican, IOR, kwa kuzingatia sheria na kanuni za Benki hii imemteuwa Wakili Ernst Von Freyberg mwenye umri wa miaka 55 kuwa Rais wa Benki ya Vatican na wajumbe wengine wanne wa Bodi wataendelea na nyadhifa zao kama kawaida. Uteuzi huu umeridhiwa na Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita.

Mchakato na hatimaye, uteuzi wa Rais wa Benki ya Vatican umefanywa kwa uangalifu mkubwa kwa kuzingatia vigezo vya: maadili, sheria, ukweli, uwazi, tija, ufanisi na weledi, kama alivyobainisha Padre Federico Lombardi, msemaji mkuu wa Vatican, wakati akizungumza na waandishi wa Habari mjini Vatican. Mchakato huu umefanywa na Wakala wa kimataifa anayejitegemea kwa kuwasilisha majina kadhaa na hatimaye jina la Wakili Ernst likateuliwa. Ni mtu mwenye uzoefu mkubwa katika shughuli za Kibenki na masuala ya Kanisa.







All the contents on this site are copyrighted ©.