Rais Traian Basescu akutana na Papa Benedikto XVI mjini Vatican
Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, Ijumaa, tarehe 15 Februari 2013 amekutana
na kuzungumza na Rais Traian Basescu wa Romania ambaye pia alikutana na viongozi waandamizi
kutoka Vatican chini ya Kardinali Tarcisio Bertone, Katibu mkuu wa Vatican.
Viongozi
hawa wawili wamefanya mazungumzo yao katika hali ya kirafiki kwa kuangalia uhusiano
kati ya Vatican na Romania, lakini zaidi uhusiano huu katika ngazi ya Bara la Ulaya,
kama sehemu ya mchakato unaopania kulinda na kudumisha tunu msingi za maisha ya binadamu.
Wamegusia pia mafanikio na matarajio ya ushirikiano kati ya Kanisa Katoliki na Serikali
ya Romania katika sekta ya elimu.
Rais Basescu kwa niaba ya wananchi wa Romania
amemshukuru Baba Mtakatifu kwa mchango wake kwa Kanisa Katoliki kama Khalifa wa Mtakatifu
Petro. Amekuwa ni msaada mkubwa kwa maendeleo ya Waamini wa Kanisa Katoliki kutoka
ndani na nje ya Romania.