Rais Obama anamshukuru na kumwombea Baba Mtakatifu Benedikto XVI
Baada ya Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita kutamka kwamba, anang'atuka kutoka
madarakani hapo tarehe 28 Februari 2013, Rais Barack Obama, kwa niaba ya wananchi
wa Marekani pamoja na Familia yake amempongeza Baba Mtakatifu kwa kusema kwamba, anamsindikiza
kwa njia ya sala.
Rais Obama anaikumbuka ile siku walipokutana na Baba Mtakatifu
mjini Vatican kunako mwaka 2009. Katika kipindi cha miaka minne, ameridhika na ushirikiano
ambao wameoneshana katika miaka hii.
Rais Obama anasema kwamba, Kanisa linatoa
mchango mkubwa nchini Marekani na katika Ulimwengu kwa ujumla. Anamtakia kila la kheri
Baba Mtakatifu pamoja na kuwaombea Makardinali watakaokusanyika kwa ajili ya kumchagua
Papa mwingine.