Huduma za Benki kwa njia ya mtandao zaanza kufanya kazi tena mjini Vatican
Huduma za Kibenki kwa njia ya mtandao zilizokuwa zimesitishwa hivi karibuni mjini
Vatican kwa sasa zimerudishwa na kwamba, mahujaji, watalii na watumiaji wa huduma
za Kibenki mjini Vatican wataweza tena kupata huduma hizi bila shida. Kwa sasa huduma
za kibenki kwa njia ya mtandao zinaratibiwa na Shirika la Aduno kutoka Uswiss.
Hayo
yamebainishwa na Padre Federico Lombardi, msemaji mkuu wa Vatican wakati alipokuwa
anazungumza na waandishi wa Habari siku ya Jumanne, tarehe 12 Februari 2013. Amefafanua
kwamba, watumiaji wa huduma za Benki kwa njia ya mtandao wataweza pia kulipia kwa
njia ya Kadi za Benki wakati watakapokuwa wanatembelea Makumbusho ya Vatican. Shirika
la Aduno linasemekana kuwa na uzoefu mkubwa katika shughuli za Kibenki Barani Ulaya.