2013-02-07 15:03:44

Ushoga ni kinyume na mpango wa Mungu.


Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Familia, Askofu Mkuu Vincenzo Paglia, ameungana na Maaskofu wa Uingereza kupinga kupitishwa kwa pendekezo la Waziri Mkuu Cameron, linalotaka kuhalalisha ndoa za mashoga, licha ya upinzani mkubwa uliopo. Jumatano Chama cha Conservatives cha Uingereza kilipitisha pendekezo hilo, na hivyo kutoa nafasi kwa muswada huo, kusonga mbele katika hatua ya kutajwa bungeni mwezi May mwaka huu.
Askofu Mkuu Vincenzo Paglia, akizungumzia pendekezo hilo, amesema, kwanza kabisa anaungana na Maaskofu wa Uingereza kupinga uhalalishaji wa ndoa za mashoga , kama pia alivyo onyesha mshikamano wake na Maaskofu wa Ufaransa kupinga sheria hiyo, ambayo pia inapigwa na watu watu wote wenye mapenzi mema wa kila dini wakiwemo Wayahudi, Waislamu,na imani za kijadi.
Askofu Mkuu Paglia, ameutaja msimamo wa Kanisa Katoliki kwamba, u wazi, ndoa huundwa na watu wawili wa jinsia tofauti mwanamme na mwanamke na si vinginevyo. RealAudioMP3







All the contents on this site are copyrighted ©.