Umoja wa Mataifa walaani mauaji ya Bwana Chokri Belaid
Kamishina wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Navi Pillay amelaani mauaji ya Bwana
Chokri Belaid, Katibu mkuu wa Chama cha Democratic Patriots Movement ambaye alikuwa
ni kati ya wanaharakati wakuu wa upinzani nchini Tunisia, kiongozi aliyesimama kidete
kulinda na kutetea haki msingi za binadamu pamoja na kuendeleza mchakato wa demokrasia
nchini mwake.
Bi Pillay anasema, mauaji yake ni pigo kubwa katika kukuza na
kudumisha demokrasia ya kweli nchini Tunisia, ambayo kwa sasa imeingia katika cheche
za machafuko makubwa kutokana na ukosefu wa haki msingi za binadamu. Bwana Chokri
Belaid alipigwa risasi Jumatano, tarehe 6 Februari 2013 alipokuwa anatoka nyumbani
kwake kuelekea kazini.
Kaminisha wa haki za binadamu anawaalika wananchi na
wapeneda amani nchini Tunisia, kuungana pamoja kupinga siasa za mauaji zinazolenga
kuwafumba mdomo wapinzani katika harakati za kutetea na kulinda haki msingi za binadamu.
Marehemu Belaid ataendelea kukumbukwa kutoka na mchango wake katika kulinda na kutetea
haki msingi za binadamu.