2013-02-07 15:32:24

Tumaini na uhai wa Kanisa ni kwa Vijana - Papa


Kwa muda wa siku tatu, Baraza la Kipapa kwa ajili ya Utamaduni, linafanya Mkutano wake wa mwaka ulioanza tarehe 6-9 Februri 2013, , katika Ukumbi Mkuu wa Chuo Kikuu cha LUMSA, Mtaa wa Borgo Sant’Angeli namba 13 hapa Roma. Mkutano unafanyika chini ya uongozi wa Mkuu wa Baraza hilo, Kardinali Ginafranco Ravasi.
Maudhui ya mkutano yanalenga zaidi katika umuhimu wa Kanisa kuwasikiliza vijana kujifunza lugha yao na kuzingatia thamani yao katika upendeleo wa kukutana na Kristu. Na pia umuhimu wa kutoa nafasi kwa vijana hata ndani ya utendaji wa kanisa. Na Kanisa kuingia katika utamaduni mpya wa tarakimu. Na hivyo, baraza limefungua Mkutano wake na Tamasha la Muziki wa Rock.

Alhamis hii, Papa alikutana na wajumbe wa Mkutano huo. Na katika hotuba yake, ameonyesha kufurahia maudhui ya mkutano huu unaochambua na kulenga kuelewa nia na lugha ya vijana na kuimarisha yaliyo mema , katika mitazamo tofauti tofauti inayojitokeza katika utamaduni wa vijana. RealAudioMP3 "








All the contents on this site are copyrighted ©.