Rais Barack Obama wa Marekani kwa mara ya kwanza kama Rais wa Marekani anatarajiwa
kufanya ziara ya kikazi nchini Israeli, mwishoni mwa Mwezi Machi 2013. Kati ya mambo
anayotarajiwa kuzungumza pamoja na mwenyeji wake ni suala la Iran, Syria na umuhimu
wa kuendeleza majadiliano kati ya Israeli na Palestina. Hayo yamebainishwa na Bwana
Daniel Shapiro, Balozi wa Marekani nchini Israeli, hapo tarehe 6 Februari 2013.
Hizi
ni juhudi za Rais Obama kuendeleza majadiliano na Iran kuhusu silaha za kinyuklia
zinazomilikiwa na Iran, ambazo zimekuwa ni tishio kwa amani na usalama wa Jumuiya
ya Kimataifa. Changamoto kubwa kwa sasa ni kuendeleza juhudi za kidiplomasia, shinikizo
la kiuchumi pamoja na Iran kuwekewa vikwazo vya kiuchumi, ikiwa kama njia nyingine
zote zitashindikana.
Kuhusu Syria, bado kuna haja kwa Jumuiya ya Kimataifa
kuhakikisha kwamba, inatumia kila njia inayowezekana ili kupata ufumbuzi wa mgogoro
wa kivita unaoendelea nchini Syria na madhara yake kwa sasa ni makubwa. Ziara hii
ya kikzazi ya siku tatu, itamwezesha pia Rais Obama kukutana na viongozi wa Palestina
na Jordan.