2013-02-05 07:56:30

DRC inahitaji kuwa na Tume huru ya uchaguzi


Viongozi wa kidini nchini DRC wanaitaka Serikali kuunda Tume huru ya Uchaguzi, kama sehemu ya mchakato wa utawala bora. Wito huu umetolewa Padre Donatien Shole, Katibu mkuu msaidizi Baraza la Maaskofu Katoliki DRC, wakati wa majadiliano kuhusu marekebisho ya sheria yanayopania maboresho ya Tume ya Uchaguzi nchini humo, ili kuwezesha uchaguzi kuwa huru na wa haki.

Viongozi wa kidini wanamwomba Rais Joseph Kabila ambaye ana mamlaka ya kuweza kusukuma wazo hili na hatimaye likafanyiwa kazi na Bunge, kwani wananchi wa DRC wanataka Tume huru inayojitegemea na itakayokuwa ni kwa ajili ya masilahi ya wengi badala mwelekeo wa sasa kuonekana kuwa ni kwa ajili ya Chama Tawala. Tume ya uchaguzi nchini humo, ilitupiwa lawama kali wakati wa uchaguzi mkuu uliofanyika kunako Mwaka 2011.

Muswada wa sheria uliopendekezwa hauna masilahi kwa wananchi wa DRC wanasema viongozi hawa wa kidini.







All the contents on this site are copyrighted ©.