Mama Clinton abwaga manyanga baada ya utumishi wa miaka minne!
Hillary Clinton aliyekuwa Katibu wa Nchi Marekani, ameng'atuka kutoka madarakani na
nafasi yake inachukuliwa na John Kerry ambaye amepanga kufanya mkutano wa ngazi ya
juu kuhusu hali tete inayoendelea nchini Syria, lakini hakufafanua zaidi.
Katika
hotuba yake, Clinton ambaye amekuwa madarakani kwa kipindi cha miaka minne amekiri
kwamba, kufanya kazi katika idara hii nyeti inayohusu uhusiano wa kimataifa imekuwa
ni heshima kubwa sana kwake. Lakini, Jumuiya ya Kimataifa inaishi katika wakati mgumu
kutokana na kushamiri kwa vitendo vya kigaidi, vinavyotishia amani na usalama wa watu,
kama ilivyojitokeza hivi karibuni kwa shambulizi dhidi ya Ubalozi wa Marekani Ankara,
nchini Uturuki.