2013-02-04 15:42:46

Kamati ya CEC yaanza kikao chake.


Jumatatu hii umeanza Mkutano wa Kamati ya pamoja ya Makanisa ya Ulaya (CEC) mjini Warszawa, katika Kituo cha Caritas cha Poland, ambako wajumbe kutoka makanisa 120 zikiwemo jumuiya za Kiotodosi , na Kipotestanti, na Halmashauri ya Baraza la Mabaraza Katoliki ya Ulaya (CCEE) wameungana pamoja. .
Mada kuu ya Mkutano ni "Imani na dini katika Ulaya inayobadilika. Jumuiya mpya za Kikristo barani Ulaya ni changamoto au nafasi . Mkutano huu unatajwa kuwa ni fursa kwa makanisa kutazama hali halisi na kutafakari kwa pamoja , juu ya mabadiliko yanayofanyika katika uhusiano mtu wa Ulaya na Mungu, na uzoefu wake wa kidini, na hasa ongezeko la jumuiya za Kiinjili za Kipentekoste Ulaya.
Kwa kuzingatia upana wa Mada , mkutano utazamishwa zaidi katika kutazama uhusiano hadi matatizo ya kihistoria kwa makanisa na vikundi vipya vya kikanisa , katika uwepo wake barani Ulaya, katika mtazamo wa kama ni changamoto mpya au ni nafasi mpya za Uinjilishaji.
Mandhari ya mkutano itaendelea kutegenezwa na michango itakayotolewa na watalaamu, zaidi ya yote, matazamio ya kijamii na kihistoria, kwa msaada wa Profesa Eileen Barker wa Shule ya Uchumi London. Watalaam wengine ni Profesa Stanisław Wargacki wa Chuo Kikuu Katoliki cha Lublin; Na Kardinali Angelo Bagnasco, Askofu Mkuu wa Genoa na pia Makamu wa Rais CCEE, pamoja na Askofu Mkuu Metropolitan Yusufu wa Patriarki wa Kanisa la Kiotodox la Romania, ambao watalenga zaidi katika uzoefu wa makanisa ya jadi yalivyo weza kudumu hadi mfumko wa makundi mapya ya kikanisa. Pia Mstaafu Askofu Mkuu wa Southwark, Kevin McDonald, na Claire Sixt-Gateuille mchungaji wa Kanisa la Reformed la Ufaransa, watalenga zaidi katika kufafanua changamoto za kichungaji.
Katika mkutano huo, washiriki watapewa taarifa za mahusiano ya Wakristu na uekumene katiak uzoefu wa Poland, kama ilivyoandaliwa na Askofu Krzyszrof Nitkiewicz, na Askofu Mkuu Jeremiasz, rais wa Baraza la Makanisa nchini Poland.
umatano Februari 6, mkutano utakamilika kwa wajumbe kufanya ziara katika jengo la Makumbusho Maasi, wakitangulwia na kauli mbili: "Mwaka wa Imani, maadhimisho ya miaka 50 ya Pili wa Vatican Baraza na Sinodi kwa Uinjilishaji Mpya" Wajibu wa CEC katika Ulaya inayobadilika , Matazamio mapya, Maono na Misioni ".









All the contents on this site are copyrighted ©.