Wafungwa 58 wafariki dunia nchini Venezuela kwa kushambuliana
Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, ametuma salam za rambi rambi kwa Askofu
mkuu Antonio Josè Lopez Castillo wa Jimbo kuu la Barquisimeto, Venezuela, kutokana
na vifo vya watu 58 vilivyotokea hivi karibuni kwenye jela ya Uribana nchini humo,
wakati wafungwa waliposhambuliana na Askari Magereza pamoja na kupelekea wafungwa
wengine 90 kujeruhiwa vibaya.
Baba Mtakatifu katika ujumbe huu ambao umeandikwa
kwa niaba yake na Kardinali Tarcisio Bertone, Katibu mkuu wa Vatican, anawasihi viongozi
na taasisi mbali mbali nchini Venezuela, kuendelea kushirikiana katika mchakato wa
kuleta maboresho ya maisha kwa wafungwa magerezani na kwamba, matukio kama haya yanayopelekea
watu kupoteza maisha yao, hajajirudii tena kwa siku za usoni.