2013-01-30 10:27:06

Viongozi wa Israeli na Vatican wakutana mjini Yerusalemu


Tume ya kudumu ya pamoja kati ya Israeli na Vatican, tarehe 29 Januari 2013 imemaliza mkutano wake wa pamoja. Monsinyo Ettore Balestrero, Katibu mwambata wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa mjini Vatican ndiye aliyeongoza ujumbe wa Vatican na kwa upande wa Israeli, alikuwa ni Bwana Daniel Ayalon, Waziri mdogo wa nchi za nje wa Serikali ya Israeli.

Ujumbe wa Vatican umetoa pongezi za dhati kwa wenzao wa Israeli kwa majadiliano ambayo yanalenga kujenga na kudumisha mafao ya pande hizi mbili. Kwa pamoja wamechambua mafanikio yaliyokwisha kupatikana hadi sasa na wanatazamia kwamba, Makubaliano haya yataweza kufikiwa muafaka mapema iwezekanavyo. Tume hii itakutana tena mwezi Juni 2013 hapa mjini Vatican.







All the contents on this site are copyrighted ©.