FAO: kuna hatari ya kuzuka tena kwa Ugonjwa wa Mafua ya Ndege!
Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa, FAO linaonya kwamba, ikiwa kama
Jumuiya ya Kimataifa haitachukua hatua za dharura, kuna uwezekano mkubwa kwamba, ikakumbwa
tena na ugonjwa wa mafua ya ndege uliotikisa dunia kunako mwaka 2006.
Hii
inatokana na ukweli kwamba, kwa sasa FAO inakabiliwa na ukata wa kuweza kupambana
na ugonjwa wa Mafua ya Ndege kutokana na athari za myumbo wa uchumi kimataifa. Serikali
zinapaswa kuwa makini ili kudhibiti dalili za kuibuka tena kwa ugonjwa wa Mafua ya
ndege uliosababisha hasara kubwa, huko Asia na Mashariki ya Kati.
Hii ni changamoto
kwa Jumuiya ya Kimataifa kuwekeza katika mikakati inayopania kudhibiti ugonjwa huu,
ambao kati ya mwaka 2003 hadi mwaka 2011: kuku na bata millioni 400 walikufa na hivyo
kusababisha hasara ya dolla za kimarekani billioni 20. Viongozi wa Jumuiya ya Kimataifa
wasipoonesha utashi wa kisiasa, ugonjwa wa Mafua ya Ndege utalipuka tena!