2013-01-29 07:19:35

Patriaki Bechara Boutros Rai kutoa tafakari ya Njia ya Msalaba kuzunguka Magofu ya Colosseo, Ijumaa kuu, 2013


Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, akiwa bado na kumbu kumbu hai ya hija yake ya kichungaji nchini Lebanon ili kuzindua matunda ya Sinodi ya Maaskofu Katoliki Mashariki ya Kati, ameamua kumkabidhi tafakari ya Njia ya Msalaba wakati wa Ijumaa kuu usiku, kuzunguka Magofu ya Colosseo mjini Roma, Patriaki Bechara Boutros Rai.

Hii itakuwa ni fursa nyingine kwa Mama Kanisa kufanya Njia ya Msalaba na Waamini wanaoishi Mashariki ya Kati, ili kuonja matumaini, mateso na mahangaiko yao ya kila siku. Taarifa ya uteuzi huu inafafanua kwamba, tafakari hii, itaandaliwa na vijana wawili kutoka Lebanon ina watafuata Vituo vya Njia ya Msalaba kadiri ya Mapokeo ya Kanisa, yaani Vituo 14.

Itakumbukwa kwamba, kwa mwaka huu, 2013, Ijumaa kuu, Siku kuu ya Mateso na Kifo cha Kristo Msalabani, itaadhimishwa hapo tarehe 29 Machi 2013.








All the contents on this site are copyrighted ©.