Kumbu kumbu ya miaka 100 ya Padre Werebrief Van Straaten, Mwanzilishi wa Shirika la
Msaada kwa Makanisa hitaji
Shirika la Kipapa kwa ajili ya Makanisa hitaji hapo tarehe 31 Januari 2013, litaadhimisha
Ibada ya Misa Takatifu kwa ajili ya kumkumbuka Hayati Padre Werenfried Van Straaten,
siku ambayo aliitupa mkono dunia, yapata Karne moja iliyopita.
Maadhimisho
ya Mwaka huu ni muhimu sana kutokana na ukweli kwamba, Mama Kanisa anamshukuru Hayati
Padre Werenfried kutokana na ujasiri wake uliosaidia kuanzisha Shirika hili ambalo
limekuwa ni msaada mkubwa kwa wanafunzi kutoka katika nchi za kimissionari wanaosoma
na kuishi hapa mjini Roma; limeendelea kutoa msaada wa hali na mali kwa Makanisa yanayodhulumiwa
sehemu mbali mbali za dunia.
Ibada ya Misa takatifu itaadhimishwa kwenye Kanisa
kuu la Bikira Maria Trastevere. Kutakuwepo na wawakilishi kutoka Bielorussia, Cuba,
Nigeria na Pakistan na itaongozwa na Monsinyo Sante Babolin, Rais wa Shirika la Kipapa
kwa ajili ya Makanisa hitaji, nchini Italia.