Bajeti kwa Ofisi ya Rais, Majeshi, Ulinzi na Usalama nchini Angola bado ni kubwa mno!
Taarifa kutoka nchini Angola zinabainisha kwamba, Bunge la Angola limepitisha bajeti
ya kiasi cha kwanza trillioni 6.6, sawa na kiasi cha dolla za Kimarekani billioni
69, sawa na ongezeko la asilimia 50% za Bajeti ya Serikali, ikilinganishwa na mwaka
2012.
Kiasi cha asilimi 33.5% ya bajeti nzima kitatumika katika sekta ya:
afya, elimu, miundo mbinu, ujenzi wa makazi kwa wananchi maskini nchini Angola, utunzaji
wa mazingira pamoja na huduma za kijamii.
Wachunguzi wa bajeti nchini Angola
wanasema kwamba, kiasi cha fedha kilichotengwa kwa ajili ya matumizi ya Ofisi ya Rais,
Majeshi, Ulinzi na Usalama bado ni kiwango cha juu kabisa, ikilinganishwa na fedha
ya bajeti iliyotengwa kwa maendeleo ya jamii na huduma kwa raia.