2013-01-26 10:42:19

Nchi za Amerika ya Kati, S.I.C.A zinathamini mchango wa Vatican katika mchakato wa maendeleo endelevu!


Askofu mkuu Luigi Pezzuto, Balozi wa Vatican nchini El Salvador pamoja na Dr. Juan Daniel Aleman Gurdian, katibu mkuu wa Mfumo wa Maendeleo Amerika ya Kati, S.I.C.A, wametiliana sahihi Mkataba unaoifanya Vatican kuwa ni nchi mwanachama mtazamaji kutoka nje ya Amerika ya Kati.

Tukio hili limehudhuriwa na mabalozi pamoja na wawakilishi wa nchi za Amerika ya Kati, hapo tarehe 21 januari 2013. Huu ni utekelezaji wa maamuzi yaliyotolewa na Wakuu wa Serikali wanachama wa S.I.C.A kwa kuruhusu Vatican kuwa nchi mwanachama kutokana na mchango wake katika mchakato wa kumletea mwanadamu maendeleo endelevu: kiroho na kimwili; dhamana inayotekelezwa na Makanisa mahalia katika sekta ya elimu, afya, jamii, utamaduni, haki, amani na usalama wa kidemokrasia.







All the contents on this site are copyrighted ©.