Mahakama ya Kitume ya Rota Romana yazindua kipindi kipya cha mwaka wa Kazi
Mamlaka ya Mahakama ya Kitume ya Kanisa Katoliki , yanayojuliakna kwa jina Rota Romana,
Jumamosi yalizindua kazi za mwaka huu, kwa Ibada ya Misa ya Ekaristi iliyo ongozwa
na Karidnali Tarcisio Bertone , katika Kikanisa cha Paolina. Kardinali Tarcisio,
katika homilia yake, aliwataka wajumbe wa Mahakama ya Rota Romana, kuwa kama walivyokuwa
watanguzi wao, kutazama sana maonyo ya Mtakatifu Paulo na kuwa na ujasiri wa kutenda
kwa haki na ukweli wa Kanisa, bila ya kuonea haya, shuhuda za Kanisa la Kristu na
kuwa wavumilivu wa kutegemea "nguvu ya Mungu kama ilivyoandikwa katika waraka wa
Mtume Paulo kwa Timoteo " (2 Tim 1:08),
Na kwamba katika dunia ya nyakati
hizi, ambayo kwa bahati mbaya imemezwa na vita, familia kuvurugwa na chuki na uadui,
wengi wakiwa wamechoka na kukosa imani, kila mtu sasa anaitwa na Kanisa kutangaza
amani na haki ya Mungu katika Kristo Yesu. Na ni kufikisha popote huduma na kazi
za kitume za Kanisa zinazo onyesha ishara ya Ufalme wa Mungu, kwa wale wanaompokea
Kristu. Ni huduma ya kutoa kila kitu bure na kuwapa wote kwa bure: upendo na huruma
ya Kristu. K Kardinali alieleza na kuweka bayana kwamba, wao si mabwana wa Neno
wanalo lihubiri, wala watu wanaowahubiria. Lakini wao ni watumishi wa mmoja kwa mwingine
, wakizifanya kazi kwa nia na neema ya Mungu kwa ajii ya wote, kwa ajili ya kuokoa
kila mmoja kwa gharama ya mwingine. Ni Kuishi na utambuzi huu kama matokeo ya
tabia ya utendaji wa kila siku, ikimaanisha , kutengeneza nafasi kwa ajili ya uwepo
wa utendaji unaoongozwa na Roho Mtakatifu, aktiak utendaji wa haki na ukweli. Kardinali
alimaliza kwa kuomba Msaada wa Mama Mtakatifu Sana Bikira Maria, Mama wa Kanisa,
Bibi arusi wa Roho Mtakatifu na kupitia nguvu ya maombezi yake, dhabihu walizotolea
katika Ibada, ziweza kuwapa zawadi ya hekima na akili, ili daima wapokee na kufanywa
upya mantiki ya kweli wa Injili, kigezo pekee katika utoaji wa hukumu za kweli na
huruma.