Papa anaungana na watetezi wa zawadi ya uhai kwa njia ya Twitter katika maandamano
nchini Marekani
Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, amewaandikia waandamaji wote wanaoshiriki
katika maandamano ya kutetea zawadi ya uhai nchini Marekani, akiwahakikishia uwepo
wake kwa njia ya sala na kwamba, anawaombea wanasiasa wote watakaosimama kidete kutetea
watoto ambao hawajazaliwa pamoja na kudumisha utamaduni wa uhai.
Ujumbe wa
Baba Mtakatifu unafanya rejea kwenye maandamano ya kutetea zawadi ya uhai, tukio ambalo
linafanyika kila mwaka ifikapo tarehe 25 Januari kwa kuwashirikisha wanaharakati wanaoendelea
kusimama kidete kulinda na kutetea zawadi ya uhai dhidi ya utamaduni wa kifo. Itakumbukwa
kwamba, ni tukio linaloungwa mkono pia na Kanisa Katoliki nchini Marekani. Kwa mara
ya kwanza tukio hili lilifanyika kunako mwaka 1973 kupinga hukumu iliyotolewa na Mahakama
kuu ya Marekani kuruhusu utoaji mimba.
Baba Mtakatifu anaendelea kujimwaga
katika matumizi ya mitandao ya kijamii kwa njia ya ujumbe mfupi, kama sehemu ya mkakati
wake wa kuinjilisha hata mitandao hii ili iweze kuwa ni jukwaa la majadiliano ya tunu
msingi za maisha na kweli za Kiinjili.