Jumapli ya wiki hii 27 Januari, itakuwa ni adhimisho la 60 la Siku ya dunia kwa ajili
ya maradhi ya Ukoma, maradhi ya tangu kale yanayoendelea kutesa watu duniani. Wagonjwa
wanao tengwa na kudharirishwa na hali ngumu za umaskini, kutokana na hali yao. Kwa
ajili hii, Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Kazi za Kichungaji kwa Wahudumu wa
Afya, Askofu Mkuu Zygmunt Zimowiski, ametoa ujumbe kwa ajili ya maadhimisho haya akisema
ni Maadhimisho ya Wakristo wote, na kuomba misaada kwa watu wenye mapenzi mema, na
kukuza dhamira zao katika kushirikiana na wagonjwa wa maradhi haya ya hatari na familia
zao, na lengo la kukuza upya kasi ya kuwaunganisha na jamii. Kwa mujibu wa takwimu
za WHO za 2011, jumla ya watu 220,000 wakiwa ni wanaume, wanawake na watoto wanaishi
na vijidudu vinavyosababisha ukoma, wengi wao wametambuliwa wakati ugonjwa umefika
katika kiwango cha hali ya juu. Askofu Mkuu Zimowski ameyataja maradhi haya kuwa
ni kati ya mijeledi halisi dhidi ya binadamu, katika baadhi ya maeneo ya dunia, yanayohitaji
ushirikiano wa Kimataifa katika utoaji wa kipaumbele kwa ajili ya kukabiliana nayo
kama ilivyokuwa katika maradhi mengine sugu homa dengue, malale, kichocho na upofu.
Na katika mwanga wa Mwaka wa imani, juhudi zaidi za kidharura zinatakiwa kuchukuliwa
na hasa Wakatoliki, katika kutimiza wajibu wao wa kuhudumia wahitaji, kama Yesumwwenyewe
alivyoagiza, nendeni mkapozeni wagonjwa , fufueni wafu , takaseni wenye ukoma, toeni
pepo, mmpewa bure toeni bure. Askofu Mkuu Zimowski ameeleza na kutoa upya mwaliko
katika maadhimisho haya ya 60 ya Siku ya Dunia ya mapambano dhidi ya ukoma, pia kama
nafasi mpya ya kuimarisha huduma ya upendo katika jamii, kw akufuata mfano wa Msamaria
Mwema, anayetajwa katika Injili.