Barua mbili binafsi za Papa kuhusu seminari na Katekesi zimechapishwa rasmi.
Ijumaa hii, kumechapishwa barua mbili binafsi za Kitume za Baba Mtakatifu Benedkto
XV1( Motu Proprio), ambazo zinahamisha mamlaka ya seminari kutoka Shirika kwa ajili
ya Elimu Katoliki, na kuingia katika shirika kwa ajili ya Mapadre. Na mamlaka yanayosimamia
Katekesi kutoka katika shirika la Makreli, na kuingia katika Shirika la Kipapa kwa
ajili ya Ukuzaji wa Uinjilishaji Mpya . Barua hizo mbili zilitangazwa na Papa
Oktoba 27, 2009, wakati wa kukamilika kwa Sinodi juu ya Uinjilishaji mpya. Wakati
wa kutangaza nia hizo mbili Papa alisema, "Katika mazingira ya tafakari za Sinodi
ya Maaskofu," Uinjilishaji Mpya kwa uenezaji wa Imani ya Kikristo, "na katika kufunga
mchakato wa kutafakari juu ya mandhari ya semina na Katekesi, na baada ya kutolea
sala na tafakari za kina zaidi , nimeamua kutangaza kwamba, kuna haja ya kufanya
mabadiliko ya kuhamisha mamlaka yanayosimamia Seminari kutoka Shirika la Elimu Katoliki,
yahamie katika Shirika la Makreli. Na pia Mamlaka yanayosimamia Katekesi, ihame kutoka
shirika la Mapadre na kuingia katika Baraza la Kipapa kwa ajili ya Kukuza Uinjilishaji
Mpya . Barua hizo mbili zilizoandikwa na Papa katika lugha ya Kilatini, zimetathmini
umuhimu wa malezi ya kipadre katika umuhimu wake kama Makuhani wa Bwana. Kwa mtazamo
huo, barua ya kitume ya Papa , inatoa dhamana kwa Shirika la Mapadre ,kusimamia kazi
zote zinazohusiana mafunzo, maisha na huduma za kichungaji katika miito ya Mashemasi
na Mapadre na uteuzi wa wale wanaowania kujiunga na Madaraja Matakatifu, yakiwemo
pia masomo yao ya kawaida na ya kiroho , mafundisho ya Kanisa na kazi za kichungaji
seminarini na katika vituo vingine kwa ajili ya mashemasi wa kudumu, na katika kuiendeleza
elimu yao, pamoja na hali ya halisi za maisha na taratibu kwa ajili ya huduma na
usalama wao katika jamii. "
Kwa barua mpya juu ya seminari, Shirika la Elimu
Katoliki, lililokuwa likishughulika na seminari na Taasisi za Elimu kwa sasa linapata
jina jipya " Mamlaka ya Elimu ya Falsafa na Tauhidi , kama ilivyoshauriwa na Shirika
la Mapadre.