Ufuatao ni wasifu wa Marehemu Padre Joachim Minja Ndelianaruwa, C.PP.S. Bwana Iongoze
miguu yetu katika njia ya amani, ndiyo iliyokuwa kauli mbiu ya maisha na utume wa
Kimissionari na Kipadre ndani ya Shirika la Wamissionari Wa Damu Azizi ya Yesu, Vikarieti
ya Tanzania. Marehemu Pd. Joachim alizaliwa mnamo tarehe 14/04/1966 – MARANGU, MOSHI,
Parokia ya MARANGU - MAKOMU, Moshi Vijijini, Jimbo Katoliki la Moshi. Ni mtoto
wa Mzee Ignasi Ndesingo Lemnge na Mama Maristella Ngelyakyau. Alibatizwa tarehe 9
Mei 1966 Parokia ya Marangu, Makomu, Jimbo Katoliki Moshi. Akapata Komunyo ya kwanza
hapo tarehe 26 Machi 1978, Parokiani Marangu na Kuimarishwa kwa Sakramenti ya Kipaimara
hapo tarehe 23 Novemba 1978 katika Parokia ya Mbahe, Arisi, Jimbo Katoliki Moshi. ELIMU
YA MSINGI: Shule ya msingi Komalyangoe iliyopo Marangu, Moshi, Mwaka 1976 - 1982. ELIMU
YA SEKONDARI; Sekondari ya LAKE iliyopo Mwanza – 1983 – 1986. Na kidato cha Tano
na Sita katika Sekondari ya Mzumbe iliyopo Morogoro kati ya mwaka 1987 - 1989. Malezi
ya wito wa Kimissionari na Kipadre Marehemu Padre Joachim Ndelianaruwa alilifahamu
Shirika akisoma Mzumbe Morogoro na akapata nafasi ya kuhudhuria semina ya wito iliyoendeshwa
na mlezi wa miito pale Bigwa Unitas – Morogoro mwaka 1987. Mnamo mwaka 1991 alijiunga
na nyumba ya malezi Miyuji – Dodoma kwa malezi ya kwanza. Mwaka 1992 hadi mwaka
1994 alisoma Falsafa katika Seminari kuu ya Kibosho iliyopo Jimbo la Moshi. Mwaka
1994 hadi 1995 – alirudi Dodoma katika nyumba ya malezi kwa ajili ya mwaka wa pili
wa Malezi. Mnamo mwaka 1995 hadi 1998 alipelekwa Morogoro kwa ajili ya masomo ya Taalimungu. Kunako
tarehe Mosi Mei, 1997 alipewa huduma ya Usomaji Altareni na Askofu Telesphor Mkude
wa Jimbo Katoliki, Morogoro. Tarehe 2 Mei 1998 akapata huduma ya Utumishi wa Altare,
kwenye nyumba ya Malezi, Miyuji, Jimbo Katoliki Dodoma. Alipelekwa Mwaka wa mazoezi
ya kichungaji, Parokia ya Itigi, Jimbo Katoliki Singida kati ya Mwaka 1998 – 1999. Marehemu
Padre Joachim Ndelianaruwa alipokelewa Shirikani, Rasmi na Daima katika SHIRIKA LA
WAMISIONARI WA DAMU TAKATIFU YA YESU, tarehe 21/10/1999 na Hayati Padre Antonio Calabrese,
C.PP.S., katika Seminari ya Mt. Gaspar Del Bufalo – Morogoro. Alipata daraja la ushemasi
wa mpito 12/12/1999 mikononi mwa Askofu Telesphor Mkude wa Jimbo Katoliki Morogoro. Marehemu
Pd. Joachim alipewa Daraja Takatifu la Upadre tarehe 07/07/2000 katika nyumba ya Shirika
iliyoko ALBANO LAZIALE - Roma, Italia na MWADHAMA POLYCARP KARDINALI PENGO, Askofu
mkuu wa Jimbo kuu la DAR ES SALAAM. Marehemu Padre Joachim Ndelianaruwa akaadhimisha
Misa yake ya Shukrani tarehe 16/08/2000 katika Parokia ya Marangu – Makomu, Jimbo
Katoliki Moshi. UTUME. Kati ya Septemba 1999 mpaka Novemba 2001 akafanya utume
wake kama Paroko msaidizi – Parokia ya Mtakatifu Nicholaus, Kunduchi Mtongani, Jimbo
Kuu la Dar es Salaam. Kati ya Novemba 2001 mpaka Juni 2002 akafanya utume kama
Msaidizi wa Procurator - Vikarieti ya Tanzania Kati ya Juni 2002 mpaka Juni 2006
akachagulia kuwa Mchumi wa Vikarieti ya Tanzania. Kati ya Juni 2006 mpaka Juni
2010 alichaguliwa kuwa Mkuu wa Shirika Vikarieti ya Tanzania. Kati ya Juni 2010
mpaka anafikwa na mauti Januari 22, 2012 alikuwa akifanya utume katika Parokia na
Kituo cha Hija cha Mtakatifu Gaspari del Bufalo, Mbezi Beach, Jimbo Kuu la Dar Es
Salaam. Pia alikuwa akisoma shahada ya kwanza ya Sheria katika Chuo Kikuu cha Tumaini,
Tawi la Dar Es Salaam. UGONJWA: Tarehe 20.01.2013 alianza kujisikia (Vibaya kiafya)
akiumwa baada ya huduma za Jumapili ( aliadhimisha misa mbili ya kwanza na ya pili)
baada ya huduma za kichungaji alikwenda kuangalia afya na alipata huduma za kimaabara
- (katika Dispensari ya Dr Hiza) na aligundulika kuwa na ugonjwa wa Malaria na kuanza
kutumia dawa za kutibu ugonwa huo. UMAUTI: umauti ulimfik Pd. Joakim Ndelianaruwa
siku ya Jumanne saa 12:10-15 asubuhi Tarehe 22.01.2013, katika nyumba ya Mapadre Mbezi
Beach. UCHUNGUZI WA KITAALAMU: Baada ya Kifo chake uchunguzi ulifanyika na kuonesha
kuwa alikuwa pia akisumbuliwa na homa ya mapafu kitaalamu PNEUMONIA. Hivyo pamoja
na shida ya malaria vikasababisha kifo chake. APUMZIKE KWA AMANI. AMINA ”LAKINI
TUNA HAZINA HII KATIKA VYOMBO VYA UDONGO”. Maneno haya yapatikana katika kadi yake
ya upadrisho.
Raha ya milele umpe Ee Bwana na mwanga wa milele umwangazie.
Apumzike kwa amani. Amina. FR. REGINALD MROSSO, C.PP.S – MKUU WA SHIRIKA - VIKARIETI
YA TANZANIA. 24/01/2013