2013-01-24 07:49:41

Siku ya Saba ya Kuombea Umoja wa Wakristo: kutembea katika mshikamano!


Katika siku hii ya saba ya kuombea Umoja wa Wakristo, wazo letu kuu ni kutembea katika mshikamano. Kwenda kwa unyenyekevu na Mungu maana kutembea katika mshikamano na wote ambao wanapambana kwa bidii kuleta haki na amani. RealAudioMP3
Hii inawapa changamoto wote ambao wanasali kuombea umoja wa kanisa wiki hii kujiuliza: Je, umoja tunaoutafuta ni kitu gani? Tume ya Imani na Madaraja, ambayo ni pamoja na wanachama wa Baraza la Makanisa Ulimwenguni likiwemo pia Kanisa Katoliki, inauelewa umoja kama umoja unaoonekana katika imani moja na katika ushirika mmoja wa Ekaristi.
Umoja huu wa kiekumene, umejitolea kwa ajili ya kuvishinda vikwazo vya kihistoria na vya sasa vinavyowagawanya Wakristo, lakini unafanya hivyo ukitazama umoja huu unaoonekana unaounganisha asili na utume wa kanisa katika huduma kwa watu ikishinda madhara yanayoweza kutokea kumdhalilisha mtu na kutusambaratisha.
Kama Tume ilivyosema: Kanisa, linaitwa na lina mamlaka ya kushiriki mateso ikiwatetea na kuwatunza maskini, wahitaji, na waliotengwa. Hii inahitaji kuainisha na kuziweka wazi miundo na kuzibadili. Kazi hii ya ushuhuda ni ya wakristu wote. Lazima kujitolea kwa ajili ya Injili hata kama kuna mateso. Kanisa linaitwa kuponya na kupatanisha mahusiano mabovu. Linaitwa kuwa chombo cha upatanisho katikati ya migawanyiko na chuki wanayosababisha watu. Hii ndiyo asili na kazi ya Kanisa.


Kuna mifano mingi ya vitendo hivyo wa uponyaji na upatanisho katika makanisa yetu. Mifano inayotukumbusha hali za dhuluma na namna ya kupambana nayo hasa zile zinazowakandamiza wanawake. Hata katika Biblia tunaona mfano wa binti ya Zelophehad ambaye Musa alimuomba Mungu ili apewe haki zake. Wanyonge wanayo haki ya kudai kujaliwa na kutunzwa.
Mfano mzuri wa Kanisa likiwa limeungana pamoja na wanaonewa ni mfano alioutoa Yesu wa msamaria mwema. Msamaria mwema akiwa mtu anayewakilisha Jamii iliyotengwa lakini anaweza kumsaidia mhitaji. Anakuwa ni chanzo cha matumaini na faraja ya kienjili. Kutembea kwa pamoja kikristo hakuwezi kutenganishwa na kutembea kwa unyenyekevu na Mungu tukitafuta haki, ukarimu na wema.

SALA
Mungu Mtakatifu katika nafsi tatu kwa njia ya maisha yako unatupa mfano wa pekee wa kukutegemea, wa upendo na mshikamano. Utuunganishe tuishi namna hii. Tufundishe kushiriki matumaini tunayoyakuta ndani ya watu wanaopambana katika maisha duniani kote. Tunaomba uvumilvu wao utuhamasishe kushinda mgawanyiko ili tuishi tumepatana sisi kwa sisi na kutembea pamoja kwa umoja. Mungu wa uzima tuongoze kwenye njia ya haki na amani. Amina.

MASWALI
Ni akina nani katika jamii yako wanahitaji mshikamano wa Jumuiya ya Kikristo?
Ni Makanisa gani yamekuwa na mshikamano na wewe?

Ni kwa njia umoja unaoonekana wa Wakristo unaimarisha mshikamano wa umoja wa Kanisa kwa wale wanaohitaji haki, ukarimu na wema katika mazingira yako?
Tafakari hii imeandaliwa na Padre Emmanuel Nyaumba.








All the contents on this site are copyrighted ©.