Zaidi ya watu millioni 197 hawana fursa za ajira duniani
Shirika la Kazi Duniani, ILO, katika taarifa ya mwenendo wa ajira duniani kwa kipindi
cha miaka mitano inaonesha kwamba, watu wengi wanaendelea kukabiliana na ukosefu wa
fursa za ajira, kwa kipindi cha miaka mitano sasa kutokana na athari za myumo wa uchumi
kimataifa.
Katika kipindi cha Mwaka 2012, idadi ya watu wasiokuwa na ajira
duniani imeongezeka kwa asilimia 5.9%, ambao ni watu millioni 4.2. Shirika la Kazi
Duniani linasema, kwa sasa kuna zaidi ya watu millioni 197 wasiokuwa na ajira. Waathirika
wakubwa ni wananchi wanaotoka katika Nchi zilizoendelea zaidi duniani. Kuna dalili
za kukua kwa uchumi kwa nchi zilizoko Asia na Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Hayo
yamebainishwa na Bwana Guy Ryder, Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Kazi Duniani. Sera
mbaya kuhusu soko la ajira zimepelekea watu wengi kukosa fursa za ajira, changamoto
ya kuwekeza zaidi kwa vijana. Hata hivyo ukuaji wa uchumi kimataifa bado unaendelea
kusua sua kiasi kwamba, haitakuwa rahisi kwa kipindi cha muda mfupi Jumuiya ya Kimataifa
kuweza kutoa ajira kwa watu millioni 210 wanaotafuta ajira.
Kuna vijana zaidi
ya millioni 74 wenye umri kati ya miaka 15 hadi 24 hawana fursa ya ajira duniani.
Wote hawa ni sawa na asilimia 12.6%.