Umoja wa Wakristo unahitaji: sala, haki na ukarimu!
Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, anaendelea kutoa changamoto chanya kuhusu
matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii, kwa kuunganisha mapokeo na mambo ya kisasa;
kwa kutumia lugha ya maendeleo ya sayansi na teknolojia ya habari pamoja na lugha
ya Kilatini, ambayo wengi walidhani kwamba, imekufa na haina tena nafasi katika Karne
ya Ishirini na moja.
Hadi sasa akaunti ya Baba Mtakatifu inawafuasi zaidi ya
Millioni mbili na nusu, wanaoendelea kuwasiliana kwa lugha ya: Kiingereza, Kiarabu,
Kifaransa, Kijerumani, Kireno, Kipolandi na hivi karibuni, “amejimwaga kwenye mtandao
kwa kutumia lugha ya Kilatini, kwa kusema kwamba, kwa hakika mtandao wa Twitter kuwa
ni mtandao unaotumia maneno machache, lakini ujumbe unafika kwa walengwa.
“Tuus
adventus in paginam publicam Summi Pontificis Benedicti XVI breviloquentis optatissimus
est” Kwa Lugha ya Kiswahili kwa msaada ya Wazee waliosoma Seminari kuu ya
Katigondo, Uganda, tunaweza kusema, “Uwepo wako rasmi Papa Benedikto XVI katika ukurasa
wa mtandao wa Twitter ni jambo la kupendeza”.
Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi
na sita, katika Juma hili la kuombea Umoja wa wakristo anabainisha kwamba, Umoja wa
Wakristo unahitaji sala, haki na utashi wa kutembea pamoja na Mwenyezi Mungu.