Mali inakabiliwa na hali ngumu ya maisha kutokana na vita inayoendelea Kaskazini mwa
nchi hiyo!
Askofu mkuu Jean Zerbo, Rais wa Shirika la Misaada la Kanisa Katoliki Mali anaiomba
Jumuiya ya Kimataifa kusaidia kutoa msaada wa dharura kwa wananchi wa Mali wanaokabiliwa
na vita baada ya Ufaransa na nchi kadhaa za Afrika kutuma vikosi vya ulinzi na usalama
nchini humo ili kupambana na vikosi vya kigaidi vinavishikilia eneo la Kaskazini mwa
Mali.
Hadi sasa watu zaidi ya watu 400,000 wameyakimbia makazi yao kwa kuhofia
usalama wa maisha na mali zao baada ya mapambano ya silaha kupamba moto Kaskazini
mwa Mali. Mwaka 2012 zaidi ya watu millioni 18 walikuwa wanakabiliwa na baa la njaa
kutokana na ukame wa muda mrefu. Ongezeko la wakimbizi na watu wasiokuwa na makazi,
linaweza kusababisha tena ukosefu wa chakula, hali inayoweza kuitumbukiza Mali hata
katika magonjwa ya mlipuko.
Caritas Mali inahitaji msaada wa dharura kutoka
katika Mashirika ya Misaada Kimataifa na Kikanda, ili kuweza kukabiliana na hali ngumu
inayowakabili watu wengi nchini humo kwa sasa na kwa siku za usoni. Baadhi ya wananchi
wamekimbilia Niger, Burkina Faso na Mauritania.