2013-01-19 07:55:14

Juma la kuombea Umoja wa Wakristo: Siku ya Pili: Kutembea na Mwili wa Kristo unaoteseka


TAFAKARI: Katika siku hii ya pili ya kuombea Umoja wa Wakristo, wazo letu kuu ni kutembea na mwili wa Kristo unaoteseka. RealAudioMP3
Kuwa wanyenyekevu kwa Mungu maana yake kusikiliza wito unaotuita kutoka katika sehemu zetu binafsi ya kujistarehesha na kuwasindikiza wengine hasa wanaoteseka. Maneno ya nabii Ezekiel yanatoa onjeleo ya hali ya maisha ya watu wengi. Mifupa yetu imekauka na matumaini yetu yametoweka. Tumetengwa. Hata katika maisha yetu nyumbani mateso yapo yanayotuvunja moyo. Ni kama yale ya Kristo msulubiwa mfuasi wa Kristo anayashiriki.
Watu wa kila nyakati na mataifa wanaoumizwa, Yesu analia kwa ajili yao: Mungu wangu Mungu wangu mbona umeniacha? Wakristo wanaitwa kuishi Njia hii ya Msalaba. Barua kwa Waebrania inaelezea thamani ya mateso ya Yesu katika wokovu wakati wa shida nyumbani na ugenini. Yesu anawaita waungane naye. Tunapokutana na wale waliotengwa, tunamtambua Mungu katika mateso yake.
Dira tunayoielekea ni sahihi na wazi. Kuwa na Kristo maana yake kuwa katika mshikamano hai na wale wanaoteseka. Ndio hawa ambamo Yesu anashiriki mateso yao. Mwili wa Kristo uliopondeka msalabani kwa ajili yako. Maisha ya mateso ya Yesu yametanguliwa na karamu ya mwisho. Na hiyo inasherehekewa kama kama ushindi juu ya mauti katika kila ibada takatifu ya Misa yaani Ekaristi. Katika adhimisho hili la kikristo Mwili wa Kristo mpondeka unafufuka katika hali ya mwili wa utukufu. Mwili wake unamegwa ili sisi tuweze kushiriki maisha yake na ndani yake tunakuwa kitu kimoja.
Kama Wakristo tunaotembea kuelekea umoja tunaweza daima kuona Ekaristi kama sehemu ambapo dhambi ya mgawanyiko ni ya kweli. Tukijua kwamba hatuwezi sisi kushiriki sakramenti hii pamoja kama tunavyopaswa. Hali hii inatuita kutafuta nguvu mpya katika mahusiano yetu sisi kwa sisi.
Somo la leo linafungua namna nyingine ya kutafakari. Kutembea na Mwili unaoteseka wa Kristo, yaani na wenye dhiki, kunafungua umoja wa kiekaristi; kushiriki mkate mmoja na walio na njaa, unavunja ukuta wa umaskini na ubaguzi, haya pia ni matendo ya kiekaristi. Ambamo wakristo wote wanaitwa kushiriki na kufanya kazi pamoja.
Papa Benedikto wa kumi na sita anaongelea tafakari yake juu ya Ekaristi kwa ajili ya Kanisa namna hii. Hiyo ni Sakramenti siyo tu kwa ajili ya kuamini bali kusherehekewa pia (Sakramenti ya upendo). Tukizingatia maana halisi ya liturjia tunang’amua kwamba hakuna kitu ambacho ni cha kibinadamu kisichorandana na maisha ya kiekaristi.

SALA
Ee Mungu wa huruma, mwana wako alikufa msalabani ili migawanyiko yetu iweze kuunganishwa. Bado tumemsulibisha mara nyingi kwa kutengana, kwa mifumo na matendo yanayozuia upendo wako na haki yako kwa wale wote ambao wamezuiwa kuona zawadi ya uumbaji wako. Umtume roho wako mtakatifu atuvuvie maisha na kutuponya na utengangano na mmeguko huu ili tuweze kushuhudia pamoja haki na upendo wa Kristo. Tembea nasi hadi ile siku tutakaposhiriki mkate mmoja na kikombe kimoja katika meza yako. Mungu wa uzima utuongoze katika njia ya haki na amani. Amina.
MASWALI
Kwa taswira ya Manabii ambamo Mungu ametaka haki, kuliko ibada zisizokuwa na haki tunahitaji kujiuliza maswali: Ni kwa jinsi gani Ekaristi, fumbo la sadaka ya Kristo na maisha mapya, linalosherehekewa kila mahali tulipo?
Je, tunapaswa kufanya nini kama wakristu kwa pamoja kushuhudia umoja wetu katika Kristo katika sehemu zinazohitaji msaada wetu wa kuziinua kutoka hali zao duni?








All the contents on this site are copyrighted ©.