Patriaki Ibrahim Isaac Sidrak ateuliwa kuliongoza Kanisa Katoliki la kikoptik la Alessandria,
Misri
Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, ameridhia uteuzi wa Patriaki Ibrahim Isaac
Sidrak, aliyechaguliwa kisheria na Sinodi hapo tarehe 15 Januari 2013 kuwa Patriaki
wa Kanisa Katoliki la Kikoptiki la Alessandria, Misri.
Sinodi ya Maaskofu
wa Kikoptiki ilikuwa na kikao chake huko Cairo, Misri kuanzia tarehe 12 hadi tarehe
16 Januari 2013, baada ya Kardinali Antonios Naguib Patriaki wa Alessandria kung'atuka
madarakani kutokana na sheria za Kanisa, Baba Mtakatifu pia ameridhia uamuzi huu.
Kabla
ya uteuzi huu, Patriaki Ibrahim Isaac Sidrak alikuwa ni Askofu wa Jimbo Katoliki la
Kikoptiki la Minya, Misri, kufuatia uteuzi uliofanywa kunako tarehe 5 Oktoba 2002
na kuwekwa wakfu tarehe 15 Novemba 2002.