Mheshimiwa Padre Andrè Gueye ateuliwa kuwa Askofu Mpya wa Jimbo Katoliki la Thiès,
Senegal
Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, amemteua Mheshimiwa Padre Andrè Gueye kutoka
Jimbo Katoliki Thiès kuwa Askofu mpya wa Jimbo Katoliki Thiès, nchini Senegal. Hadi
uteuzi wake, Askofu mteule alikuwa ni Jaalim wa Falsafa katika Seminari kuu ya St.
Jean Marie Vianney iliyoko Jimbo Katoliki la Ziguinchor, Senegal.
Askofu mteule
Andrè Gueye alizaliwa tarehe 6 Januari 1967, Jimboni Thiès, Senegal. Baada ya masomo
na majiundo yake nchini Senegal na Roma, kunako tarehe 27 Juni 1992 akapewa Daraja
Takatifu la Upadre. Tangu wakati huo ametekeleza utume wake wa Kipadre kama Paroko
msaidizi, Paroko, na Jaalim. Jimbo Katoliki la Thiès lilikuwa wazi tangu mwaka 2011
kutokana na kifo cha Askofu Sacques Sarr.