2013-01-07 09:26:53

Umoja wa Afrika wapongeza uamuzi uliofikiwa kati ya Sudan ya Kusini na Sudan Kongwe


Dr. Nkosanza Dlamini Zuma, Kamishina wa Umoja wa Afrika amepongeza uamuzi wa pamoja uliofikiwa kati Rais Omar Hassan Al Bashiri na Rais Salva Kiir Mayardit katika mkutano wao uliofanyika mjini Addis Ababa, kuanzia tarehe 4 hadi tarehe 5 Januari 2013, chini ya usimamizi na uongozi wa Rais mstaafu wa Afrika ya Kusini, Thabo Mbeki ambaye aliteuliwa kuwa ni mpatanishi katika mgogoro wa pande hizi mbili.

Umoja wa Afrika unaendelea kusisitizia umuhimu wa viongozi wa nchi hizi mbili kutekeleza kwa vitendo mambo msingi yaliyofikiwa katika mkutano wao uliofanyika kunako tarehe 27 Septemba 2012 kuhusu mipaka ya nchi hizi mbili. Lengo ni kuimarisha misingi ya haki, amani na maendeleo endelevu, kwa kuwajengea wananchi wa Sudani ya Kusini na Sudan Kongwe ari na moyo wa kujiamini katika mchakato wa kujiletea maendeleo endelevu; wakishirikiana kwa pamoja ili kutafuta mafao ya wengi, katika nchi hizi na Bara la Afrika, katika ujumla wake.







All the contents on this site are copyrighted ©.