Toeni muda wenu kwa wahitaji na Mungu, Papa amehimiza.
Baba Mtakatifu Benedikto XV1,Jumatatu Usiku aliongoza Kanisa la Ulimwengu, kusherehekea
Siku Kuu ya Kuzaliwa kwa Bwana wa Noel , kwa kuongoza ibada ya Mkesha wa Noel katika
Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro. Ibada iliyohudhuriwa na maelfu ya waamini na kutangazwa
katika vyombo vya mawasiliano duniani kote. Papa akitoa mahubiri katika Ibada
hiyo, alitoa swali kwa waamini na wasioamini, iwapo wanapata nafasi katika maisha
yao nyenye hekaheka na shughuli nyingi, maisha yanayoendeshwa na teknolojia, nafasi
kwa ajili ya watoto na maskini na Mungu?