Twitter: Ukitaka kutembea katika mwanga, jitahidi kuongozwa na Neno la Mungu; furaha
ya kweli inapatikana kwa kuungana na Mungu!
Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita mara baada ya Katekesi Jumatano tarehe 19
Desemba 2012, ametuma ujumbe wake kwa njia ya mtandao wa kijamii wa twitter akisema
kwamba, hija ya imani ina nyakati kuu mbili: mwanga na giza. Kama mwamini anapenda
kutembea daima katika mwanga, basi haja budi kuongozwa na Neno la Mungu.
Sehemu
ya pili ya twitter ya Baba Mtakatifu inasema kwamba, Bikira Maria aliweza kufurahia
ujumbe kwamba, atakuwa ni Mama wa Yesu, Neno wa Mungu aliyefanyika mwili. Anasema,
furaha ya kweli inajikita katika kuungana na Mwenyezi Mungu.
Hii ni twitter
na sita kutumwa na Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, tangu alipozindua matumizi
ya mtandao huu wa kijamii, ambao hadi sasa una zaidi ya wafuasi millioni mbili na
sabini elfu. Wafuasi katika akaunti ya Baba Mtakatifu @ Pontifex kwa lugha ya Kiingereza
wamekwisha vuka millioni moja na laki mbili; kwa lugha ya Kihispania kuna wafuasi
465,000 na katika lugha ya Kitaalia kuna wafuasi 200,000.