2012-12-15 15:06:18

Tahariri ya Padre Lombardi . tendeni kwa amani


Tahariri ya Padre Federico Lombardi kwa wiki hii, imetazamishwa katika Ujumbe wa Papa kwa ajili ya siku ya Amani Duniani, 1 Januari 2013. Ujumbe wenye jina "Heri wapatanishi," kama ilivyoandikwa katika Injili. Wale ambao kwa imani kwa Mungu na ahadi zake "mara nyingi hubezwa au kupuuzwa na walimwengu. Lakini Papa anasema, watu hao huweza kuuonja uzoefu wa maisha ya furaha kama zawadi toka kwa Mungu.
Padre Lombardi, ana ainisha kwamba, Ujumbe wa Papa unakwenda kinyume na mitazamo mingi ya kileo. Unatoa msisitizo kwamba, "sharti la amani" ni "kuvunja udikteta wa itikadi na dhania za kutoamini Mungu, zenye kuzuia utambuzi wa sheria asili ya maadili, iliyoandikwa na Mungu katika dhamiri ya kila mtu." Hivyo ujumbe, anarudia kuangalisha juu ya utetezi wa maisha , ndoa na juu ya uhuru na haki katika daku za utambuzi.
Na si tu katika mazingira ya mgogoro wa kipeo cha sasa, mnamo sisitizwa kazi za kijamii kitaifa, haki ya kufanya kazi ,lakini katika ukweli wake, tatizo la njaa ni baya zaidi kuliko hata kipeo cha fedha , na juu ya umuhimu wa kuwa na mfumo wa maendeleo, usiotanguliza juu faida na maslahi binafsi lakini utendaji kwa ajili manufaa ya wote, na kuthamini zawadi asilia zinazopatikana bure.
Kwa amani, tunaweza kuelimika na kuwa na muono wa mbele zaidi juu ya familia, shule na jumuiya za kidini na kiraia, pamoja na ufundishaji wa kweli na umakini katika utoaji wa maneno, ishara na mitazamo.
Miaka hamsini iliyopita, Papa Yohane XXIII, ilitoa waraka wake maarufu "Amani Duniani ,(Pacem in Terris)" akisema, “ nguzo ya amani ni ukweli, uhuru, upendo na haki”. Amani ni utaratibu usio tangamana na upendo. Hivyo inakuwa ni kufikiria mahitaji ya wengine na kufanya sehemu na mali zao , kuwa sehemu yetu pia.
Pengine yote haya yanaonekana kama ndoto , lakini sisi wote tunajua kwamba ni haki. Hebu tujaribu tena, amemalizia Padre Lombardi.








All the contents on this site are copyrighted ©.