2012-12-15 15:28:34

Kardinali Filoni akutana na Waseminaristi wa Jimbola Arua.


Kardinali Leonardo Filoni , Ijumaa akiwa Uganda pia alipata nafasi ya kuwatembelea Seminaristi wa Arua. Katika hotuba yake , alilenga katika swali jepesi , nini lengo la kuwa seminarini au kwa maneno mengine ya kueleweka zaidi nini maana ya majiundo haya katika mwelekeo wa kuwa kuhani.
Alitoa ufafanuzi kwa maswali hayo, akiangalisha katika Injili ya Mtakatifu Marko, juu ya kuzaliwa kwa jumuiya ya kitume, kama ilivyoandikwa katika sura ya tatu , ambamo Yesu aliteua kumi na wawili ... Yesu anaunda jumuiya mpya , kitendo cha ubunifu na kuwaunda ili waweze kuwa pamoja nae na ili aweze kuwatuma kwenda kuhubiri Injili .
Katika muktadha huu wa imani, basi, ni muhimu kuwa na taarifa na uelewa, kuwa na akili wazi na kujifunza, kukumbuka daima utu wa Yesu Kristo, asili ya ukweli na kweli.
Na alihitimisha hotuba yake kwa kuwashirikisha furaha za utakatifu katika kuwa wanafunzi wa Yesu, wenye kuwa na hamu ya kutambua wito wake. Awali ya yote,alisema, ni kukuza na kuwa na upendo mkubwa kwa Yesu Kristo katika Sakramenti hii ya Ukuhani. Heri wao wanaoingia katika utumishi wa Sakramenti hii! Yeye sasa ni kweli katika Ekaristi, hivyo ni kujitahidi kujifunza na kumjua vizuri zaidi na kubaki katika umoja naye, na kutenda kila jambo kwa Imani kubwa kwake.
Pili, daima kuwa waaminifu kwa Kanisa na Mafundisho yake – na daima kuufanya upendo wake ujulikane , kuwa tayari kubeba ushahidi wake, hata katika majitoleo ya sadaka ya utakatifu wa kuifia dini, mbele ya watu . Hatimaye, mwe watu jasiri na imara wa Mungu, katika hali zote, kwa sababu maisha ya kikristo ni jambo zuri! (Taz. Flp 4., 4).
Kardinali alikamilisha hotuba yake kwa kutoa swali kwa wote, kama mseminaristi ataka ukuhani wa aina gani? Je ni kuhani anaye mshuhudia Kristo kwa sababu anaamini, anampenda, na ndiye anayemwonyesha hatua za utendaji katika maisha? Ni aina gani ya kuhani anataka kuwa kwa ajili ya Kanisa, baada ya nusu karne ya Mtaguzo Mkuu wa Pili wa Vatican. Je ni tayari kuchukua urithi alioupata kwa kujengwa kwa njia ya kazi ngumu na umwagaji wa damu, isiyokuwa na hatia ya mashahidi wengi, wamisionari watakatifu, na wake kwa waume wa Imani? Je, Kristo na Kanisa ni matumaini yake? Ni kujiuliza, Je, mimi kweli miko tayari kuwatumikia katika daraja hili la ukuhani kwa usafi wa moyo, kama zawadi ya jumla ya Kristo? Je, nina moyo wa Kristo kujenga kanisa na kufanya uinjilishaji katika karne ya Ishirini na moja. Jibu unalo wewe, alisema Kardinali Filoni .







All the contents on this site are copyrighted ©.