Rev. Dr. Jovitus Mwijage ateuliwa kuwa Mkurugenzi wa PMS Tanzania
Kardinali Fernando Filoni, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Uinjilishaji wa watu
amemteua Mheshimiwa Padre Jovitus Mwijage kutoka Jimbo Katoliki Bukoba kuwa Mkurugenzi
wa Mashirika ya Kipapa ya Kazi za Kimissionari nchini Tanzania kwa kipindi kuanzia
mwaka 2012 hadi mwaka 2017.
Uteuzi huu umeanza kutekelezwa hapo tarehe 23
Novemba 2012. Mheshimiwa Padre Mwijage alizaliwa kunako tarehe 2 Desemba 1966. Alipadrishwa
takribani miaka kumi na saba iliyopita. Baada ya kufanya utume mbali mbali kama Paroko
usu, mhasibu na mlezi wa Seminari Ndogo ya Rubya Bukoba, alipelekwa mjini Roma kuendelea
na masomo na hatimaye kujipatia Shahada ya Uzamivu kuhusiana na Historia ya Kanisa
kutoka katika Chuo Kikuu cha Kipapa cha Gregorian.