Watumiaji wa mitandao ya kijamii! Kumekucha mjini Vatican!
Ndugu msikilizaji wa Radio Vatican, zifuatazo ni anuani kwa lugha mbali mbali ambazo
zinakuwezesha wewe kutwitter na Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita kwa njia
ya mitandao ya kijamii. Huu ni mtandao ambao unazinduliwa rasmi tarehe 12 Desemba
2012, katika Kumbu kumbu ya Bikira Maria wa Guadalupe.
Itakumbukwa kwamba,
tukio hili liliwasilishwa kwa waandishi wa habari mjini Vatican hapo tarehe 3 Desemba
2012. Waliobahatika kuwasiliana na Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita katika
akaunti yake binafsi @pontifex watajibiwa ili kuzima kiu yao kuhusu imani.
Habari kutoka
Vatican zinabainisha kwamba, mtandao huu wa kijamii utaendelea kuongeza lugha mbali
mbali kadiri inavyowezekana. Bila shaka, iko siku moja hata watumiaji wa mitandao
ya kijamii wataweza kuwasiliana na Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita kwa kutumia
lugha ya Kiswahili, lakini kwa sasa, tuvute subira kwani mambo mazuri wanasema Waswahili
hayahitaji haraka!