2012-12-11 15:35:36

Marekani yaaswa Kanisa huanzia nyumbani


Amerika Kusini, Caribbean, Marekani na Canada ni nyumbani kwa ukatoliki, kwa kuwa nusu ya idadi ya Wakatoliki duniani iko katika eneo hilo. Hilo lilielezwa Jumatatu wakati wa kufunguliwa kwa Mkutano wa Kimataifa wa Marekani zote mbili unaofanyika kwa ajili ya maadhimisho ya kutimia kwa miaka 15 tangu kutolewa kwa hati ya Kichungaji na Mwenye Heri Yohane Paulo 11 , baada ya Sinodi ya Maaskofu iliyofanyika kwa ajili ya Kanisa barani Amerika ya Kusini na Amerika ya Kaskazini, Caribbea na Canada, mwaka 1999.

Baba Mtakatifu Benedikto XV1, akitoa hotuba wakati wa Ibada ya Misa, iliyoongozwa na Kardinali Marc Ouellet, Mkuu wa Decania ya Maaskofu Katoliki, aligusia "ukarimu i" na "roho wa umisionari, ulivyokuwa tangu mwanzo wa Kanisa katika eneo hilo. Mkutano huu unahudhuriwa na washiriki 250 kutoka eneo hilo linalojulikana kama Mabara mapya.

Kardinali Marc Ouellet, katika homilia yake wakati wa Ibada, alilitaka “Bara mpya ' kudumisha roho wa kiinjili na umisionari ulioonekana tangu Ukristu kuingia katika eneo hilo , na liwe mstari wa mbele katika Uinjilishaji Mpya. Lijibidishe katika kuimarisha juhudi za kufikisha Imani Katoliki katika maeneo ambayo bado kuguswa, Kaskaini na Kusini, kupitia juhudi za kuimarisha ushirikiano na uratibu kati ya makanisa mahalia na kujenga ustaarabu wa upendo.

Kuwe na juhudi za kulitambulisha na kuliinua Kanisa kupitia ushauri na muono wake,katika kumaliza migogoro na tofauti za kimbali itikadi, kidini na siasa, kupitia njia ya majadiliano na kuheshimu utu wa mtu, na familia ya mke na mme, na katika kujali matatizo mengine ya Kijamii. Alihimiza kipeo cha kijamii kinachoendelea sasa ni wakati muafaka wa kueneza na kuzungumzia nguvu ya Kristo, ambayo ni upendo, kwa kuanzia ndani ya familia.
Aidha aligusia suala la wahamiaji na ghasia zinazo shamirishwa na mitandao ya biashara ya madawa ya kulevya na matumizi yake ya ovyo kuongezeka. Lakini juu ya yote, Kardinali ilionyesha kujali zaidi mashambulizi dhidi ya utamaduni wa maisha na taasisi ya ndoa na familia, ambapo alielezea kama tatizo la bara zima, na haja ya kulinda uhuru wa dini.

Na Dk Guzmán Carriquiry, Katibu Mkuu wa Tume ya Kipapa kwa ajili ya Amerika ya Kusini, kitengo cha mahusiano kati ya Makanisa katika mataifa ya mabara haya, akishiriki Mkutano huu, alitaja migawanyiko inayojitokeza mara kwa mara. Na alipongeza Sinodi 1997 kwamba, ilikuwa ni ni sehemu ya kuvunja tabia ya kutilia mashaka, badala yake imefanikisha kuleta umoja zaidi kwa viongozi wa Kanisa Marekani.

Na Mlei Carl A. Anderson , Mkuu wa Chama cha Knights of Columbus, kinacho dhamini kazi za matendo ya huruma ya Papa katika mataifa ya Amerika ya Kusini, akizungumzia mabadiliko ya kiroho, alisema, uponyaji huu unapaswa kuanzia tangu katika kuelewa maana ya sakramenti ya ndoa ya Kikristu . Na haiwezekani kuendeleza utume wa Uinjilishaji Mpya , bila kwanza kutangaza kwa bidii ukweli juu ya binadamu na utu wake . Kama Wakristu tunapaswa kutangaza kwa ushupavu na ushawishi wa kweli juu ya ndoa na familia . Kwa maana hiyo , Wakristu leo hii wanaitwa katika Uinjilishaji Mpya , ambamo wao wenyewe wanatakiwa kwanza kuongoka na kuyaonyesha maisha Katoliki ya kweli.

"Kinachotakiwa ni si tu mipango mipya ya kichungaji kwa wale ambao hawaukubatii tena Ukristu , ingawa bado ni muhimu kufanya hivyo , pia tulenge zaidi kwa wale4 ambao habari hii njema ya upendo bado kuwafikia. Uinjilishaji Mpya lazima upanuke zaidi na uwe na chanya zaidi katika upeo". Aliendelea "ni kutoa ujumbe unaoongea nguvu ya Kristo, ambayo ni upendo ... kwa kuanza ndani ya familia na kuchanua hadi kwa jamii nzima kwa ujumla.

Na alionyesha kujali haja ya kidharura, juu ya watu masikini na wale wanaoteseka kwa sababu mbalimbali msingi zilizo nje ya uwezo wao. Alikumbusha nchi za Magharibi, kuwa ni maeneo yenye rutuba ya upendo na fadhila, mnamo weza kustawi tena moyo wa ubinadamu wa kuajaliana , kama ilivyokuwa karne za nyuma. Ni tu kwa kujenga ustaarabu wa upendo Wakatoliki wanaweza kuwa na mshikamano wa kweli na umoja wa kikanisa Marekani ".

Alikamilisha kwa kuangalisha katika Ujumbe wa Mama yetu ya Guadalupe na katika maisha ya St Juan Diego, i unaoonyesha dhahiri wito wenye lishe mpya ya utangazaji wa Injili kwa Kanisa zima, na kwa kila mtu na taifa.








All the contents on this site are copyrighted ©.