2012-12-08 09:10:19

Papa anaomboleza kifo cha Patriaki Ignazio wa IV Hazim


Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, ametuma salam za rambi rambi kwa Askofu mkuu Spyridon wa Jimbo kuu la Eliopoli, kufuatia kifo cha Patriaki Ignazio IV Hazim, wa Kanisa la Kigiriki la Kiothodox kwa Mashariki yote, kilichotokea hivi karibuni.

Baba Mtakatifu anaungana na wote wanaoomboleza msiba huu kwa kuondokewa na mchungaji wao mkuu kwa njia ya sala. Marehemu Patriaki Ignazio IV Hazim, enzi ya uhai wake, alijitoa katika kutangaza Injili, akaonesha ushuhuda wa mwanga angavu wa imani na mapendo; akawahimiza Wakristo wake kuchuchumilia upatanisho, haki na amani miongoni mwa Jumuiya ya Kimataifa. Ni kiongozi aliyechuchumilia kwa dhati kabisa majadiliano ya kiekumene kati ya Makanisa haya mawili, ili wote waweze kuwa wamoja chini ya Kristo.

Mwishoni, Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, anapenda kuwahakikishia waamini wote wanaoteseka kutokana na sababu mbali mbali uwepo wake wa karibu pamoja na kuendelea kuombea amani huko Mashariki ya Kati.







All the contents on this site are copyrighted ©.