2012-12-07 15:22:06

Monsinyo Georg Gànwein, Katibu muhtasi wa Papa ateuliwa kuwa Askofu mkuu


Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, amemteua Monsinyo Georg Gànswein, Katibu muhtasi wake, kuwa Askofu mkuu na Mkuu wa Nyumba ya Kipapa. Askofu mkuu mteule Ganswein alizaliwa tarehe 30 Julai 1956 nchini Ujerumani. Baada ya masomo na majiundo yake ya Kikasisi alipadrishwa kunako tarehe 31 Mei 1984.

Kunako mwaka 1993 alijiendeleza kwa masomo ya juu na hatimaye akajipatia shahada ya uzamivu kutoka Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Munich, Ujerumani. Kwa miaka kadhaa alifanya kazi kama Hakimu wa Mahakama ya Jimbo pamoja na kuwa msaidizi binafsi wa Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Freiburg im Breisgau.

Kunako mwaka 1995 alianza kufanya utume wake mjini Vatican katika Baraza la Kipapa la Ibada na Nidhamu ya Kanisa. Mwaka 1996 akahamishiwa kwenye Baraza la Kipapa la Mafundisho Tanzu ya Kanisa na huko alikuwa ni katibu muhtsasi wa Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Mafundisho Tanzu ya Kanisa. Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, alipochaguliwa kuliongoza Kanisa, akamteua Monsinyo Georg Gànswein kuwa katibu wake muhtasi.







All the contents on this site are copyrighted ©.