2012-12-01 16:50:01

Msomi Dr Patriaca, apokea tuzo ya Novak ovak A 2012.


Tuzo ya Novak 2012, ambayo hutolewa na Taasisi ya Acton, mwaka huu imenyakuliwa na Msomi, Dr Giovanni Patriarca , mwalimu katika taasisi na vyuo vya Nuremberg Ujeruman.

Dr Giovanni Patriarca, alipokea tuzo, hivi karibuni kama ilivyoandaliwa na Chuo Kikuuu cha Kipapa cha Mtakatifu Thomas wa Aquinas cha hapa Mjini Roma.

Waliowasilisha tuzo hiyo ni Padre Robert Sirico, Mkurugenzi na mwanzilishi mwenza wa Taasisi ya Acton , pia akiwepo Kishore Jayabara, Mkurugenzi katika Ofisi za Taasisi ya Acton Roma.

Tuzo ya Novak , ambayo iliitwa kwa heshima ya Mwanateolojia na mwanafilosofia katika masuala ya kijamii , Michael Novak , hutolewa kwa Msomi, aliyefanya bidii zaidi katika kuendeleza tafiti na mahusiano ya kina, katika utu wa biadamu na umuhimu wa mipaka ya kiserikali katika uhuru wa kidini na uchumi huria.

Mshindi wa tuzo hii , hupokea kiasi cha dola 10,000, na pia huwasilisha mada maalum wakati wa sherehe za kupokea tuzo, mhadhara unaojulikana kwa jina Calihan. Dr Patriaca , katika mhadara huu wa Calhan, alisisitiza juu ya ukweli wa asili ya kipeo cha uchumi kwa wakati huu.

Alisema, ingawa kipeo cha sasa katika asili yake, kinasababishwa na mambo kadhaa ya kiufundi, lakini pia, ni kutokana na mabadiliko kadhaa katika tabia za maisha ya kijamii na mahusiano kati ya mtu na mtu. Hivyo kunahitajika mabadiliko mengine , kwa ajili ya kurejesha tena utulivu. Na kwamba kati ya dalili zinazojionyesha katika mbadiliko ya sasa, ni uwajibikaji wa mtu kwa yeye binafsi, na katika mahusiano yake na wengine na kazi za umma. Mabadiliko yanayonekana kukuza moyo wa kujitenga na wengine na kupendelea zaidi ubinafsi .

Alitoa maelezo hayo kwa kurejea pia kwamba, katika vipindi vyote vya kihistoria , kumekuwa na enzi za ukosefu wa utulivu na kipindi cha mpito kinachotaguliwa na mabadiliko katika mtazamo wa kiuchumi na mahusiano ya kijiografia.

Na alionyesha kujali , umuhimu wa kuongeza jitihada katika kuyatambua leo hii mazingira ya faragha na mitazamo ya kimataifa. Na mabadiliko haya hutokea kwa mwendo wa kasi kiasi kwamba , mtu hushindwa kwenda sambamba na mabadiliko hayo na hivyo hupelekwa himahima bila ya kujitambua na bila ya kuwa na lengo mfano wa maji ya yanayo tiririka toka mlimani. Na hivyo uhuru wenyewe unakuwa bandia na huzidiwa na usasa, na hivyo binadamu hupoteza mwelekeo wa maisha yake ya ndani.

Dr. Patriarca pia alitazamisha katika ubabe na njia zisizofaa, katika demokrasia ya Magharibi, ambayo kwa sasa misingi yake katika baadhi ya haki fulani zinagandamizwa na kugeuzwa kuwa hoja.

Msomi huyo ameonya mwelekeo wa watu wa ulaya kusahau mizizI ya utamaduni wao wa tangu kale za kigriki, kirumi, kiyahudi na Kikristo, kwa kisingizio cha jina la demokrasia katika chaguzi zinazotafuta kuufunika uwazi na kweli, zilizosimikwa katika utambulisho wa utamaduni wa tangu zama za kale.
Pia ameasa dhdi ya uwepo wa imani zilizo simikwa katika anasa , zenye kuhamasisha ukosefu wa uwajibikaji, usio ruhusu kujihukumu katika lolote, iwe kujirudi kimwili au katika wito wa kiroho."Amesisitiza , uhuru wa kweli, huandamana na kutambua maana ya halisi ya uhuru , kama tabia kuu ya ubinadamu.

Patriarca alihitimisha: "Pengine katika muda huu wa ukimya na tafakari, kupitia ishara za unyenyekevu au ukali wa maisha ya kila siku, tunaweza kufurahia kwa mara nyingine, maadili halisi na kujenga tena mzunguko wa wema na maelewano, mshikamano na heshima na bila ubinafsi , kwa kuheshimiana mmoja kwa mwingine. "








All the contents on this site are copyrighted ©.