2012-12-01 09:37:32

Mikakati ya Viongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki


Rais Jakaya Mrisho Kikwete wa Tanzania amerejea nyumbani kutoka Nairobi, Kenya ambapo amehudhuria mkutano wa Viongozi wa Nchi za Jumuiya ya Africa Mashariki (EAC), mkutano ambao umehitimisha vikao na sherehe mbalimbali za kufungua miradi ya pamoja ya nchi hizi.

Katika mkutano wa tarehe 30 Novemba, 2012, Rais Mwai Kibaki wa Kenya amemkabidhi rasmi Rais Yoweri Museveni wa Uganda, Uenyekiti wa Uongozi wa Jumuiya, kikao ambacho kimehudhuriwa na viongozi wote wakuu wa Burundi, Kenya, Rwanda, Tanzania na Uganda.

Tarehe 27 Novemba, 2012 Rais Kikwete amehutubia Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki katika kikao chake cha tatu tangu kuzinduliwa rasmi mwaka huu. Rais Kikwete amesema pamoja na changamoto zilizopo, Jumuiya inazidi kukua na kuimarika.

Tarehe 28 Novemba, 2012 Viongozi wa EAC wamezindua makao ya kudumu ya ofisi za EAC, sherehe ambayo umehudhuriwa na viongozi wa nchi hizi ambapo mara baada ya uzinduzi wa jengo hilo, viongozi wote wakaelekea Athi River na kufungua rasmi barabara ya Arusha - Namanga- Athi River yenye urefu wa kilometa 240. Sherehe ambayo pia umehudhuriwa na Rais Piere Nkurunziza wa Burundi ambapo Rais Yoweri Museveni wa Uganda na Paul Kagame wa Rwanda wamewakilishwa na Mawaziri wao Wakuu. Katika ufunguzi huo, Rais Kikwete amesema Jumuiya hii ni muhimu na yenye manufaa makubwa kwa nchi hizi.

Tarehe 29 Novemba, 2012 viongozi wamekutana katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Kenyatta na kuzungumzia miradi mbalimbali ya miundombinu ikiwemo, barabara, reli na bandari , miradi ambayo kwa pamoja itahudumia na kunufaisha wananchi wa nchi hizi.








All the contents on this site are copyrighted ©.