2012-11-30 15:52:59

Ndoa ni chumbuko la uhai mpya na shule ya watoto


Maaskofu Katoliki wa New Zealand, wamewasilisha tamko lao kwa Kamati ya Kiserikali , juu ya mswada unaotaka kubadilisha maana na neno ndoa.

Tamko la Maaskofu limetaja imani yao kwamba, neno Ndoa, huonyesha kwa namna ya kipekee katika , uwajibikaji wa kudumu wa kijamii, katika mahusiano kati ya mwanamme mmoja na mwanamke mmoja , mahusiano ambayo asili yake, huelekea katika kuumba uhai mapya wa binadamu.

Maaskofu wanataka maana ya neno ndoa lilindwe kisheria, kwamba, asili ya ndoa ni muungano kati ya mwanaume na mwanamke na si vinginevyo.

Katika hati yao wameeleza kwamba, Kanisa Katoliki daima huhimiza ndoa ya mke na mme , kama ilivyo katiak asili yake ya kuwa chimbuko na kituo msingi katika maisha ya kijamii, na pia hufanikisha mazingira bora kwa ajili ya malezi ya kulisha familia na watoto. Na hivyo, utendaji wa wanandoa ndiyo msingi wa taifa kuwa na jamii bora au taifa bora.
Na hivyo Kanisa huunga mkono taasisi na mafundisho yote yanayoandaliwa kwa ajili ya wake kwa waume wanaotarajia kufunga ndoa ya mke na mme, ambamo hutolewa mada mbalimbali kama maandalizi kwao ya kujenga familia bora, na pia kuelimishwa juu ya changamoto wanazo weza kupambana nazo na jinsi ya kukabiliana na hali ngumu pale mmoja wao anapo fariki dunia au katika hali za kutaka kutengana.
Kanisa Katoliki linaweka bayana kwamba, huu si mjadala juu ya ushoga, lakini ni swala la ufafanuzi juu ya asili ya neno ndoa, kwamba ni mke na mme, ndoa inayo inadharirishwa na watu wa jinsia moja, wanaoishi pamoja, na kutaka na kupata haki ya kutambulika kama wana ndoa.
Kanisa Katoliki linarudia tena kusisitiza kwamba asili ya ndoa inatokana na watu wawili mke na mme katika asili ya tofauti zao kijinsia, kuungana pamoja kinyumba na kuuunda familia katiak muungano wao. Kanisa Katoliki linatambua haki hii ya ndoa na hakuna binadamu anayeweza kuitangua. Na kila binadamu ana haki ya kuingia katika muungano huu kwa uhuru kamili kama kutimiza asili ya maumbile.









All the contents on this site are copyrighted ©.